• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Mufindi District Council
Mufindi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Planing and Statistics Department
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara yaElimu ya Msingi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii,Jinsia na Vijana
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ujenzi
    • Kitengo
      • Kitengo cha Tehama
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Huduma za Kisheria
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na MH. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Taarifa
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Lyra yapeleka neema ya bweni shule ya sekondari Idunda

Posted on: October 21st, 2025


Shirika la LYRA limekabidhi bweni jipya katika Shule ya Sekondari Idunda, iliyopo  katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ikiwa ni hatua kubwa ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuinua ufaulu wa wanafunzi wa kike, ambapo bweni hilo limejengwa kwa lengo la kupunguza changamoto zilizokuwa zikiwakabili wanafunzi wa kike waliokuwa wakitembea umbali mrefu kufika shuleni hali iliyokuwa ikisababisha utoro na kushuka  kwa ufaulu.

Akizindua bweni hilo Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Mh. Dkt. Linda Salekwa ameishukuru LYRA  kwa mchango huo mkubwa na kuwataka walimu na wazazi kushirikiana kuhakikisha ndoto za wanafunzi wa kike na wa kiume zinatimia. huku akitoa onyo kali kwa walimu wanaojihusisha na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi ambapo amesema kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayebainika kujihusisha kimapenzi na wanafunzi.

Aidha ametoa rai kwa wazazi na walezi kutoa ushirikano wa kutosha kwa bodi ya shule na walimu kwa kuwahakikisha wanashiriki kikamilifu katika malezi ya watoto watakaoishi bweni ikiwemo upatikanaji wa chakula huku akiwasihi walimu kusimamia na kuwa walezi wa watoto  ili wapate elimu iliyokususdia badala ya kuwa sehemu ya ushawishi na kwamba mwalimu yoyote atakayebainika kuwa sehemu ya ushawishi hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Lyra in Africa Bw. Gerald Usika amesema shirika hilo kwa kushirikiana na Jamii na Serikali limekuwa likitekeleza miradi mbalimbali ya kijamii ikiwemo ujenzi wa mabweni ya wasichana katika shule za sekondari za kata zilizopo mkoani Iringa kwa lengo la kusaidia kupunguza tatizo linalowakabili watoto wa kike, kuhakikisha kuwa wako salama na kuwa na uhakika wa kumaliza kidato cha nne salama. huku akisema kuwa katika Halmashauri ya wilaya ya Mufindi imefanikiwa kufikisha mabweni matano, mawili yakiwa katika Shule ya Sekondari Kihansi, Kata ya Mapanda. moja katika shule ya sekondari ya Maduma kata ya Maduma na Moja katika shule ya sekondari Ifwagi kata ya Ifwagi.  

Akielezea utekelezaji wa bweni katika shule ya sekondari Idunda amesema limejengwa kwa kutumia ramani ya Shirika la Lyra, iliyozingatia mazingira, kuwapa wanafunzi sehemu nzuri na salama ya kuishi na kujisomea likiwa na vyumba vya kulala 13 vyenye uwezo wa kulaza jumla ya wasichana 104, chumba cha matroni pamoja na jiko na choo chake, matundu 15 ya vyoo pamoja na choo cha watu mwenye mahitaji maalumu, vyumba 11 vya bafu, eneo la kufulia nguo, eneo la kujisomea na eneo la wazi ndani ya jengo kwa ajili ya kupumzika hivyo kupelekea gharama ya ujenzi wa bweni kuwa ni Shilingi za Kitanzania. 253,873,497/=

Akitoa shukrani zake kwa uongozi mzima wa shirika la Lyra Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mufindi, Ndg. Mashaka Mfaume, amesema kabla ya mradi wa bweni kuwepo wanafunzi wa shule hiyo walilazimika kutembea zaidi ya kilomita 2 kila siku, jambo lililokuwa likisababisha utoro, uchovu na kushuka kwa ufaulu. lakini kupitia uwepo wa bweni hilo hakutakuwa na utoro lakini pia kutaongeza kiwango cha ufaulu.

 “Kupitia miradi kama hii, tunajenga taifa lenye elimu, usawa na matumaini mapya kwa watoto wa kike.” Amesema Mfaume

Hafla hiyo ya makabidhiano ya bweni hilo iliambatana na matukio mbalimbali ikiwemo utiaji saini hati ya makabidhiano ya bweni, makabidhiano ya hati, ugawaji wa vyeti kwa wadau mbalimbali walishiriki katika kufanikisha ujenzi wa bweni pamoja na upandaji miti katika eneo la bweni.





Tangazo

  • TANGAZO LA KAZI ZA MUDA MAPATO MUFINDI DC SEPT 2025 September 24, 2025
  • TANGAZO LA KAZI ZA MUDA USAFI MUFINDI DC SEPT 2025 September 25, 2025
  • ORODHA-YA-ASASI-ZILIZOPATA-KIBALI-CHA-UANGALIZI-WA-UBORESHAJI-WA-DAFTARI-MWAKA-2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA KAZI JULAI 2024 MUFINDI DC July 22, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Lyra yapeleka neema ya bweni shule ya sekondari Idunda

    October 21, 2025
  • HAKIKISHENI MAREJESHO YANAFANYWA KWA MWITIKIO MKUBWA - DAS MUFINDI

    September 25, 2025
  • Ziara yenu ikazae mbinu mpya utekelezaji program ya ECO-SCHOOLS -Kaimu DED Mufindi DC

    September 22, 2025
  • Mufindi DC yajikita zaidi kupunguza vifo vitokanavyo na changamoto za uzazi

    July 14, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA TASAF MUFINDI KAYA MASKINI
Video Nyingine

Viungio vya Haraka

  • Muongozo wa Kutumia Mfuo wa FFRAS

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Ajira za Utumishi
  • Ofisi ya Mkuu Mkoa wa Iringa
  • Hati ya Mishahara ya Watumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

https://thesiswritingservice.net/

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mufindi District Council Office

    Postal Address: 223 Mafinga

    Telephone: 026 - 2772614

    Mobile: 026 - 2772614

    Barua Pepe: ded@mufindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Onyo
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani

Copyright ©2018 Mufindi District Council. All rights reserved.